Sura: AL-QAARIAH 

Aya : 2

مَا ٱلۡقَارِعَةُ

Nini Inayo gonga?



Sura: AL-QAARIAH 

Aya : 3

وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا ٱلۡقَارِعَةُ

Na nini kitakacho kujuilisha nini Inayo gonga?



Sura: AL-QAARIAH 

Aya : 4

يَوۡمَ يَكُونُ ٱلنَّاسُ كَٱلۡفَرَاشِ ٱلۡمَبۡثُوثِ

Siku ambayo watu watakuwa kama nondo (vipepeo) walio tawanyika;



Sura: AL-QAARIAH 

Aya : 5

وَتَكُونُ ٱلۡجِبَالُ كَٱلۡعِهۡنِ ٱلۡمَنفُوشِ

Na milima itakuwa kama sufi zilizo chambuliwa!



Sura: AL-QAARIAH 

Aya : 6

فَأَمَّا مَن ثَقُلَتۡ مَوَٰزِينُهُۥ

Basi yule ambaye mizani yake itakuwa nzito,



Sura: AL-QAARIAH 

Aya : 7

فَهُوَ فِي عِيشَةٖ رَّاضِيَةٖ

Huyo atakuwa katika maisha ya kupendeza



Sura: AL-QAARIAH 

Aya : 8

وَأَمَّا مَنۡ خَفَّتۡ مَوَٰزِينُهُۥ

Na yule ambaye mizani yake itakuwa khafifu,



Sura: AL-QAARIAH 

Aya : 9

فَأُمُّهُۥ هَاوِيَةٞ

Huyo maskani yake yatakuwa Moto wa Hawiya!



Sura: AL-QAARIAH 

Aya : 10

وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا هِيَهۡ

Na nini kitacho kujuilisha nini hiyo?



Sura: AL-QAARIAH 

Aya : 11

نَارٌ حَامِيَةُۢ

Ni Moto mkali!



Sura: ATTAKAATHUR

Aya : 1

أَلۡهَىٰكُمُ ٱلتَّكَاثُرُ

Kumekushughulisheni kutafuta wingi



Sura: ATTAKAATHUR

Aya : 2

حَتَّىٰ زُرۡتُمُ ٱلۡمَقَابِرَ

Mpaka mje makaburini!



Sura: ATTAKAATHUR

Aya : 3

كَلَّا سَوۡفَ تَعۡلَمُونَ

Sivyo hivyo! Mtakuja kujua!



Sura: ATTAKAATHUR

Aya : 4

ثُمَّ كَلَّا سَوۡفَ تَعۡلَمُونَ

Tena sivyo hivyo! Mtakuja kujua!



Sura: ATTAKAATHUR

Aya : 5

كَلَّا لَوۡ تَعۡلَمُونَ عِلۡمَ ٱلۡيَقِينِ

Sivyo hivyo! Lau mngelijua kujua kwa yakini,



Sura: ATTAKAATHUR

Aya : 6

لَتَرَوُنَّ ٱلۡجَحِيمَ

Basi bila ya shaka yoyote mtaiona Jahanamu!



Sura: ATTAKAATHUR

Aya : 7

ثُمَّ لَتَرَوُنَّهَا عَيۡنَ ٱلۡيَقِينِ

Tena, bila ya shaka yoyote, mtaiona kwa jicho la yakini



Sura: ATTAKAATHUR

Aya : 8

ثُمَّ لَتُسۡـَٔلُنَّ يَوۡمَئِذٍ عَنِ ٱلنَّعِيمِ

Tena bila ya shaka yoyote mtaulizwa siku hiyo juu ya neema



Sura: AL-ASWRI 

Aya : 1

وَٱلۡعَصۡرِ

Naapa kwa Zama!



Sura: AL-ASWRI 

Aya : 2

إِنَّ ٱلۡإِنسَٰنَ لَفِي خُسۡرٍ

Hakika binaadamu bila ya shaka yumo katika khasara,



Sura: AL-ASWRI 

Aya : 3

إِلَّا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّـٰلِحَٰتِ وَتَوَاصَوۡاْ بِٱلۡحَقِّ وَتَوَاصَوۡاْ بِٱلصَّبۡرِ

Ila wale walio amini, na wakatenda mema, na wakausiana kwa haki, na wakausiana kusubiri



Sura: AL-HUMAZAH 

Aya : 1

وَيۡلٞ لِّكُلِّ هُمَزَةٖ لُّمَزَةٍ

Olewake kila safihi, msengenyaji!



Sura: AL-HUMAZAH 

Aya : 2

ٱلَّذِي جَمَعَ مَالٗا وَعَدَّدَهُۥ

Aliye kusanya mali na kuyahisabu



Sura: AL-HUMAZAH 

Aya : 3

يَحۡسَبُ أَنَّ مَالَهُۥٓ أَخۡلَدَهُۥ

Anadhani ya kuwa mali yake yatambakisha milele!



Sura: AL-HUMAZAH 

Aya : 4

كَلَّاۖ لَيُنۢبَذَنَّ فِي ٱلۡحُطَمَةِ

la hasha! Atavurumishwa katika moto hutama



Sura: AL-HUMAZAH 

Aya : 5

وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا ٱلۡحُطَمَةُ

Na nani atakujuvya ni nini moto wa hutama?



Sura: AL-HUMAZAH 

Aya : 6

نَارُ ٱللَّهِ ٱلۡمُوقَدَةُ

Moto wa Mwenyezi Mungu ulio washwa



Sura: AL-HUMAZAH 

Aya : 7

ٱلَّتِي تَطَّلِعُ عَلَى ٱلۡأَفۡـِٔدَةِ

Ambao unapanda nyoyoni



Sura: AL-HUMAZAH 

Aya : 8

إِنَّهَا عَلَيۡهِم مُّؤۡصَدَةٞ

Hakika huo utafungiwa nao



Sura: AL-HUMAZAH 

Aya : 9

فِي عَمَدٖ مُّمَدَّدَةِۭ

Kwenye nguzo zilio nyooshwa